Michezo Ya Mfalme
KSh750.00 KSh660.00
Professor Marcel Kalunga Mwela-Ubi anatokea Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na tafsiri hizi zilishinda na kupewa tuzo katika mashindano ya kutafsiri tamthilia za Kifaransa katika Kiswahili. Kwa jinsi maandiko yenyewe yalivyo na mvuto mkubwa, baada ya kusoma kurasa chache na kuzoea matumizi ya Kiswahili cha Congo (Kingwana), msomaji atazama katika uhondo wa ucheshi wa tamthilia hizi na kugundua kuwa, kumbe si lazima, waandishi wote watumie Kiswahili sanifu.
Professor Kalunga Mwela-Ubi anaandika hivi kuhusu “Michezo ya Mfalme”: Katika hadithi hii ya Victor Hugo, Mufalme ni mpenda wanawake sana na aogopi kama mwanamke mwenye anamutamania ni bibi wa mutu ao mutoto wa watu. Kikubwa kwake ni kutaka tu kujifurahisha. Triboulet, mutumwa wa Mufalme, eko na kilema mu mukongo. Kazi yake ni kumuchekesha Mufalme. Lakini na yeye pia eko na mutoto wake mwanamuke muzuri sana mwenye alimupataka na marehemu bibi yake. Triboulet anamupenda kupita vitu vyote vya pa dunia na anamuchunga muzuri sana juu asiangukie mu mutego wa Mufalme kama wanawake wengine. Lakini, ujanja wa Triboulet utaweza kweli kukawia siku nyingi? Kwa sababu ya hasira na chuki aliyokuwa nayo kwa Mufalme, Triboulet anatafuta ginsi ya kulipiza kisasi amuue Mufalme aliyefaulu kumnyanyua mutoto wake, Blanche. Mambo itakuwaje? Itawezekana, ao hasira yake itageuka kuwa hasara kwake?
Reviews
There are no reviews yet.